Sunday, September 19, 2010

WATANZANI WATIA FORA SWEDEN


na Robinson Wangaso


Na Robinson Wangaso

Waliwavuta vijana hao wa Kiswedishi hasa katika mihadhara mbalimbali ya kubadilisha mawazo na uzoefu.

WATANZANI WATIA FORA SWEDEN



waliweza kuwafurahisha vijana wenzao wa kisweden ambao pia wako katika harakati za kuja nchi Tanzania kujifunza mazingira, Tamaduni, usawa wa kijinsia na Democrasia.



Ni vijana 14 wa kitanzania

SIKU TISINI ZA MASOMONI SWEDEN.

Na Robinson Wangaso - Sweden





Hakika kutembea ni kujifunza, pampja na kuwa nilikuwa nchi Swedeni kwa ajili ya masomo lakini kuna elimu kubwa niliyoipata nje ya darasani kwa kujifunza mambo mengi yakiwemo utunzaji wa mazingira, jinsi watu wanavyojichukulia au kujiheshimu na kutojiheshimu kwa nkuwa wapo ulaya.

Kwangu kwenda ulaya siyo jambo muhimu, muhimu ni matokeo baada ya kutoka Ulaya nini nitajifunza na ni namna gani nitaweza kubadilisha hali fulani katika maisha na namna ya kusaidia jamii ya Watanzania.

Wapo walioenda mbali zaidi na hata kutaka kukana desturi zao wakidhani ulaya ndiyo mambo yote, lakini nilichokibaini ni kuwa WAZUNGU wanayo hamu kubwa ya kujifunza kutoka kila kona hata kwa WAAFRIKA ambao tumekuwa kujijidharau kila siku.

Haba baadhi ya Watanzania wakiwa nchini Sweden

Wednesday, September 15, 2010

KIKWETE UNAKUMBUKA AHADI YAKO MARA

Na Robinson Wangaso, Musoma. 0765632944/ 0712735318

Imebaki miezi mitano tu, na siyo miaka mitano ufanyike uchaguzi mkuu bila kutekelezwa kwa ahadi ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa kwa wakazi wa mkoa wa Mara ya kukamilisha ujenzi wa hospitali ya mkoa wa Mara lililopo katika eneo la Kwangwa manispaa ya Musoma kama alivyosema kwa miaka mitano Hospitali ya mkoa itakuwa imekamilika.


Akihutubia umati mkubwa katika mkutano hadhara wa kampeini mwezi Oktoba 2005 uliyohudhuriwa na wananchi wa mkoa huu kutoka wilaya zote rais Kikwete akiwa mgombea Urais kwa Tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM aliahidi kuwa mkoa hauna hospitali yenye hadhi kutokana na uliyopo kuwa na majengo chakavu na haitoshi kutokana na ongezeko la wagonjwa kwani majengo ya hospitali hiyo yalijengwa zama za mkoloni.

" Mkoa wa Mara hauna hospitali yenye hadhi ya kimkoa, hii iliyopo imepitwa na wakati. Ni ahadi yangu kwenu kwa kipindi cha miaka mitano Hospitali yenu mpya itakuwa inafanya kazi, hii ni ahadi yangu kwenu na kamwe hamtanisuta baada ya miaka mitano" alisema raisi Kikwete.

Miaka ya 1980 wananchi wa mkoa wa Mara wakiwemo wakulima ambao walikuwa wakikatwa shilingi tatu kwa kila kilo moja ya pamba ambayo ilikuwa ikiuzwa katika vyama vya ushirika kwa wakati huo walichangia kwa zaidi ya miaka mitano ujenzi wa hospitali mpya ya mkoa ambapo jengo lake halikukamilika na kuishi njiani kwa kile kinachodaiwa kuwa usimamizi na matumizi ya fedha hizo haukuwa mzuri.

Ujenzi wa Hospitali hiyo ambayo ilifikia ghorofa Tatu na kuishi hapo umekuwa ni kero kubwa ya wakazi wa mkoa wa Mara kwa serikali ambayo ilishindwa kusimamia fedha hizo za wananchi na kuwachukulia hatua wale waliokuwa wamekabidhiwa dhamana ya kusimamia ujenzi kwa niaba ya wananchi ambapo jasho la wanyonge kupotea bure bila huruma.

Kutokana na hali hiyo kuonyesha wananchi kupunguza imani na serikali yao kwa kushindwa kutimiza na kukamilisha azma ya wananchi, viongozi mbalimbali wakiwemi wale wanaowania nafasi mbalimbali za kisiasa wakiwemo wajumbe wa Halmashauri kuu ya taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM wamekuwa wakitumia kero hilo katika kampeni wakitoa ahadi ya kukamilisha ujenzi huo pindi wakichaguliwa kwa kuisukuma serikali na baada ya kuchaguliwa huishia mitini.

Kero hiyo pia alifikishiwa rais Kikwete na alichaguliwa kuwa rais aliporudi katika ziara yake ya Kwanza mkoani Mara mwezi Januari 2006 ya kushukuru wakazi wa mkoa wa Mara na wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani hapa Augosti 9 hadi 14 2006 alisema Serikali imekubaliana Kanisa Katholiki kukamilisha ujenzi huo ambao gharama za ujenzi zitatolewa kwa ushirikiano baina ya serikali na Kanisa hilo huku usimamizi wa ujenzi utakuwa chini ya kanisa.

Katika hotuba hiyo ambayo aliitoa katika viwanja hivyo hivyo vya shule ya msingi Mukendo, rais alisema hospitali hiyo itakalimishwa ujenzi wake na kufunguliwa kama hospitali ya Rufaa ili kusongeza karibu huduma ya matibabu kwa wananchi wa mkoa wa Mara na mikoa mingine ya kanda ya ziwa ambayo hawana hoaspitali za Rufaa na kuahidi kupanuliwa iliyokuwa hospitali ya mkoa ya zamani.

Wananchi wameshuhudia upanuzi ukifanyika lakini bado wanahoji, nguvu zao na michango yao ambayo waliielekeza katika ujenzi wa hospitali ya Kwangwa na kuahidiwa na viongozi wa kisiasa wakiwemo wale wa kitaifa kuwa ingekamilika zimetupwa au tena katika chaguzi zijazo ahadi zitaendelea kutolewa ambapo ni zaidi ya miaka 20 jengo hilo ambalo inasadikika limejengwa kwa ustadi mkubwa bila kukamilika.

Akionekana ni mwenye Ari, Nguvu na Kasi ya kutekeleza ahadi hiyo, rais alirudi Musoma Mwezi Agosti 31 mwaka 2006 kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa askofu wa jimbo la Musoma Mhashamu Justin Tetemu Samba ambapo alirudia kauli yake mbele ya waamini wa kanisa hilo na wananchi walijitokeza katika mazishi hayo kuwa mazungumzo na makubaliano baina yake na Askafu yalikuwa yamekamilika na hivyo aliomba msimamizi wa jimbo atakaechaguliwa na kanisa aendeleze juhudi hizo bila kuchelewesha ili serikali itoe fedha na ujenzi huo uanze.

" Mkoa wa Mara umepoteza mtu muhimu sana katika huduma za kiroho na maendeleo ya kijamii, Serikali ilikuwa na mkakati wa kushirikiana nae katika ujenzi wa Hospitali ya Rufaa mkoani hapa" alisema Rais Kikwete wakati wa salamu zake wakati wa mazishi hayo.

Mwezi Agosti 27 hadi Sepemba 1 2007 waziri mkuu wa wakati huo Edward Lowassa ambae alifanya ziara ya kikazi mkoani Mara ambae alionyesha kwa kipindi cha uongozi wake kufuatilia masuala muhimu za mkoa wa Mara yakiwemo mapigano ya koo za kabila la wakurya Tarime alifanya ziara mkoani Mara na kutembelea jengo hilo la Hospitali ikiwa ni kutaka kutekeleza ahadi ya seriakali ambapo alielezwa na msimamizi wa jimbo wa wakati huo Padre Julius Ogola kuwa kanisa lipo katika mchakato wa kuanza ujenzi tatizo ni fedha kwani ujenzi huo unagharimu fedha nyingi na serikali isaidie isaidie upatikanaji wake ili kazi ianze na waziri mkuu huyo aliahidi kuchukua hatua kwa haraka kwa ahadi hiyo ya serikali ya awamu ya nne kwa wananchi wa mkoa wa Mara.

Lowassa kaondoka madarakani, lakini najua waziri mkuu yupo na ofisi ya rais bado ipo? Je ni ninakila sababu ya kujihoji tatizo lipo wapi? serikali imesahaua ahadi zake au imedhamilia rais ili akutwe na wananchi wa mkoa wa Mara ambao ni wa wazi na wakweli wasio na soni hata kidogo baada ya miaka mitano ya serikali ya awamu ya nne kumalizika.

Wakati wa askofu mpya wa kanisa hilo Mhashamu askofu Michael Msongazila ulioyofanyika katika kanisa kuu la Maria mama wa Mungu, Lowassa alihudhuria sherehe hizo na kumshika mkono Mara baada ya kusimikwa rasmi na kumhakikishi kuwa serikali itashirikiana naye katika ujenzi wa hospitali ya rufaa. Lowassa aliondoka na serikali?


Hivi ni kweli ahadi hiyo haina kumbukumbu au kuondoka kwa Lowassa hakuna tena kiongozi wa serikali tofauti na rais kufuatilia ahadi alizotoa rais wakati wa kampeni ili zitekelezwe. Tunajua kuwa rais anazo shughuli na majukumu mengi, ndiyo maana wapo mawaziri, wakuu wa mikoa na ha wilaya ili kumsaidia kazi kutokana ma mfumo na mgawanyo wa madaraka ikiwa ni pamoja na kumkumbusha katika maeneo yao nini kinaendelea.

Kama ndiyo kwani ahadi siyo jambo muhimu kwa mkuu wa mkoa kumkumbusha rais, au tunasubiri kumpatia taarifa za matukio ya mauaji na mambo mengine huku ahadi hizo zikiwa zinakumbukwa vizuri na wananchi na wanasubiri wakati wa kampeni wamuulize "mzee ilituahaidi, ulisema kamwe hatutakuja kukusuta" ? Je rais utajibu vipi hapo?

Natumaini majukumu muhimu ya viongozi serikali katika mikoa ni pamoja na kujua wananchi wan shida gani na kipi wanamdai kiongozi wao wa kitaifa ndiyo maana ya uwakilishi na siyo kueleza mazuri tu kuwa unakubgalika mzee, je kwa nini msimwambie kuwa wananchi wanamdai nini ili watimizie.

Rais aliona umuhimu huo wa kuwa na hospitali ya mkoa ambao ni dhahili kila mmoja wetu anaukubali kutokana na huduma ya afya katika mkoa wa Mara kuwa inahitaji kupewa msukumo wa pekee kutokana na mkoa wenye wilaya sita unayo hospitali moja tu ya wilaya katika wilaya ya Tarime, huku wilaya ya Bunda wakitumia hospitali teule DDH inayomilikiwa na kanisa la KKKT, Wilaya ya Serengeti na Rorya hospitali zilizopo zinamilikiwa na kanisa la Menonite, Musoma vijijini na mjini hakuna hospitali ya wilaya na zinategemea hospitali ya mkoa.

,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,mwisho,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

BUTIAMA WAMPONGEZA JK

Na Robinson Wangaso, Musoma - MARA 0784301526, 0765632944

Wananchi wa kata za Butiama ,Masaba, Muryaza na Butuguri wilayani Musoma vijijini mkoani Mara wamefanya maandamano ya kumpongeza rais Jakaya Kikwete kwa kuiteua Butiama kuwa wilaya mpya.

Sherehe hizo zimefanyika jana kijijini Butiama katika ukumbi wa Joseph Kizurira Nyerere ambao ulishatumika kuikutanisha Halmashauri kuu ya taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM chini ya uongozi wa mwenyekiti wa chama hicho taifa Jakaya Kikwete na kutoa pendekezo la jina la Butiama kupewa wilaya mpya itakayoundwa kutoka wilaya ya Musoma vijijini.

Maandamano hayo ambayo yameanzia katika vijiji mbalimbali vya kata hizo yamepokelewa mkuu wa wilaya ya Musoma ambae aliwakilishwa na Afisa Tarafa ya Makongoro Lucy Makenge na viongozi mbalimbali waandamizi kutoka halmashauri ya wilaya.

Bi Lucy Aliwaasa wakazi wa Butiama kuwa tayari kushirikiana na kuijenga wilaya hiyo mpya ili kumuenzi Baba wa Taifa Mwali Julius Kambarage Nyerere kwa mambo mazuri aliyoyafanya katika kuongoza nchi na amewathibitishia wananchi hao kuwa saerikali ya jamuhuri ya Muungano itatimiza azma yake ya kuanzishwa na kuiendeleza wilaya mpya ya Butiama.

" Kwa niaba ya familia ya mwalimu Nyerere, anatoa shukrani kwa Rais Kikwete kwa kuona umuhimu wa kuanzisha wilaya mpya yenye jina la Butiama, kijiji alichozaliwa Baba wa Taifa" alisema Lucy, Afisa tarafa.

Akiongea kwa niaba ya wazee wa kijiji cha Butiama, Mzee Jackton Nyerere alisema " Nyerere Burito baba yake na mwalimu Nyerere kabla ya kifo chake aliwahi kutabiri kuwa Butiama itakuwa na wageni wa kila aina, kuanzishwa kwa wilaya hii ni kukamikilika kw utabiri wa Chiefu huyo wa kabila la wazanaki" alisema mzee Jackton Nyerere.

Nae Mwalimu Jack Nyamwaga alisema kikao cha Halmashauri kuu ya taifa kufanyika Butiama kilikuwa na jambo ambapo Tanzania imeweza kuazimia mabo mengi ikiwemo azimio la Arusha, siasa na kilio, Azimio la Musoma anazimio la Mwisho kwa mjibu wa mwlimu huyo ni kuanzishwa kwa wilaya mpya ya Butiama.

Hafla hizo pia zimeandaman na ngoma, kwaya, michezo mbalimbali ziikiwemo ya asili kutoka kabila la Wazanaki, Waikizu ambapo maelfu ya wananchi kutoka kata jirani na Butiama wamehudhuria.

kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Butiama Zakaria Wambura alisema Ris Kikwete amemuenzi baba wa taifa kwa vitendo kwa ambapo wilaya hiyo mpya itakuwa chachu katika kuinua hali za maisha ya wananchi wa kata hiyo na kata jirani

Wakati huo huo mmoja wa wanafamilai ya mwalimu Veronica Jackton Nyerere ametangania nia ya kuwania nafasi ya ubunge vitri maalumu mkoani Mara kupitia ambae amewataka wananchi hao kutoshangilia wilaya mpya na kuwapisha wageni, bali wafanye kazi kwa bidii.

"Wanabutiama tuwe wabunifu ili wilaya iwe wilaya mfano ya kumuenzi baba wa taifa na tukubali kubadilika na kuwasomesha watoto ili kuendana na soko la ajira" alisema Veronica Nyerere mbele ya umati huo.

,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,mwisho,,,,,,,,,,,,,,,,,,

UCHAGUZI SWEDEN

Na Robinson Wangaso, Sweden +46722071257.

Jumapili ijayo ni siku muhimu kwa Wananachi wa Sweden ikiwa ni siku ya uchaguzi wa kuwapata viongozi wao wa kisiasa katika ngazi ya majimbo, mkoa na wawakilishi katika Bunge sawa na ngazi ya kitaifa.

lakini kwa Waswidi zoezi la kupiga kura limeanza wiki moja kabla kwa wale anaodhani siku hiyo hawatakua na nafasi kwenda kupiga kura wanafika kwa wakati wao wanaopenda katika vituo vilivyopo wanapiga kuza zao na kuondoka.

Kilichonistajabisha zaidi ni pale nilipotembelea kituo kimojawapo cha kupiga kura katikati ya jiji la Stockholm ambao ndiyo mji mkuu wa nchi hii na kujionea jinsi kura hizo zinavyopigwa katika hali ya uwazi.

Japo kura ni siri lakini wakati mtu anapopiga kura yake katika eneo la kupigia kura unaweza kusogea karibu bila wasiwasi kama ilivyozoeleka nyumbani nchini Tanzania bila shaka nawe utapiga kura yako na kuondoka.

Zaidi ya hapo katika chumba cha kupigia kura nilikuta watu wawili ambao ndio wasimamizi wa upigaji kura hakuna mawakala wa vyama vya siasa na watu wanawaamini na kupiga kura zao bila kuhofia kuwa kura zitaibiwa jambo ambalo lilinishabgaza kuona hivyo tume ya uchaguzi kusimamia upigaji kura kwa kuaminiwa na wananchi pamoja na wanaogombea kupitia vyama mbalimbali vya siasa.

Kuhusu kampeni kama tunavyojua juma la mwisho huwa ni vurugu mechi lakini ukiwa nchini Sweden hutajua kua ni wiki ya Uchaguzi kama hujaambia na mtu kwani kampeni hazifanyiki katika mikutano ya hadhara bali ni kupitia vyombo vya habari na kuwasambazia majumbani vipeperushi wananchi kupitia masanduku yao ya Barua (Posta)vinavyoelezea sera za vyama vyao.

Pia katika baadhi ya niji na majiji unakuta wafuasi wachache wa vyama fulani wakigawa machapisho hayo ya sera kwa watu wanaopenda kujua juu ya chama hicho lakini kazi hiyo inafanyika katika hali ya utulivu na hakuna vurugu wala kulazimishwa kuchukua kipeperushi bali kwa kuombwa kwa lungha ya unyenyekevu kuchukua vipeperushi.

Mfumo wa uchaguzi ni kuchagua Chama na siyo mtu, kila chama kinakua na orodha ya wagombea ambao watateuliwa kuingia bungeni Mara baada ya uchaguzi ikiwa kitashinda lakini watakaoteuliwa inategemeana na asilimia ya ushindi au kura chama kilichopata.

Lakini pia mpiga kura kabla ya kupiga ataangalia orodha ya wagombea wa chama anachokipenda na ikia ataona mtu anaempenda amewekwa katika orodha nafasi ya mwisho kwa umuhimu anaweza kuzungushia jina lake kuonyesha kua mtu huyo anapenda apewe nafasi kutokana na kua anapenda aiingie Bungeni.


Pamoja na wagombea kupewa nafasi za kipaumbele na vyama vyao pia wananchi au wapiga kura wanayo fursa ya kubadilisha orodha kwa kumpigia mtu furani aliyopewa nafasi ya mwisho na kupewa nafasi kubwa ya kuteuliwa kuwawakilisha katika bunge ikia ni namna ya kuthamini na kuheshimu wanachokipenda wapiga kura.

Zaidi ya vyama Saba zinashiriki katika uchaguzi utakaofanyika Wiki hii hapa nchini Sweden huku hakuna kelele wala vurugu zozote zinazoashiria kuwepo na uchaguzi watu wakiendelea na shughuli zao kamakawaida.

Wanaoruhusiwa kupiga kura ni raia wa Swedena na wageni ambao siyo raia lakini wenye vibali (VISA) za zaidi ya miaka mitatu kuishi nchini humo nao wanayo haki ya kupiga kura hata kama siyo raia wa nchi hiyo.

Sweden ni nchi inayofuata mfumo wa utawala wa Kifalme lakini ikiwa na vyama vingi vya siasa na kiongozi mkuu na msimamizi shughuli za serikali ni waziri mkuu ambae huchaguliwa kwa kupigia kura kila baada ya miaka minne.

,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,mwisho,,,,,,,,,,,,,,,,

Thursday, June 10, 2010

MAUAJI YA WANYONGE MARA HAYAPEWI KIPAUMBELE

KUMEKUWA NA MAUAJI ya mara kwa mara Yaliyotokea katika mkoa wa Mara na mengi ya mauaji hayo kutoripotiwa kabisa katika vyombovya habari pengine ni kutokana na waandishi wa habari kutoona umuhimu ama kutofuatiliamatukio hayo sambamba na viongozi kupuuza wakiwemo makamanda wa jeshilapolisi wa kanda maalum Tarime /Rorya na mkoa wa Mara.

Kabla ya kuwanyooshea vidole viongozi hao hebu kwanza nianze na sisi wenyewe kama waandishi wa habari ambaotumekuwa tukisikia matukio ya watu kuuawa na kutofuatilia huku tukifuatilia habari za vikao na mabaraza ya madiwani na kikutano ya wabunge kwa kuwatunajua kuna posho huko.


Hivi mtu kuuawa haijalishi kipato chake, mtanzania mwenye haki na thani ya kuishi kamabinabamu anauawa usitake kuandika habari hiyo na badala yake siku hiyo unaandika habari ya mbunge ama diwani katoa ahadi ya kukarabati barabara ama kachangia ujenzi wa sekondari, kweli hiyo ndiyo dhamani tuliyonayokatika kuielimisha, kuihabarisha Jamii ya watanzania kamawana habari?

Kwa upande wa viongozi watawala na makamanda na jeshila polisi, Kuna badhi ya matukio yakitokea hujitahidi kutoa taarifa kwa waandishi hata kwa kuwatafuta kwasimu, lakini baadhi ya matukio yakiwemo mauaji wa watu wenye kipato kidogo ambao bndio watanzania halisi na walio wengi wenye mchango mkubwa katika taifa lao, wanaoiweka serikali madarakani kuupuuzwa na kutotolewa taarifa endapo hakuna mwandishi naliyefuatilia amakuuliza juu ya mauaji hayo pengine kwakutopata dokezojuu ya tukiohilo.

Viongozi na waandishi wa Habari hatuwatendei haki watanzania walio wengi.