Thursday, June 10, 2010

MAUAJI YA WANYONGE MARA HAYAPEWI KIPAUMBELE

KUMEKUWA NA MAUAJI ya mara kwa mara Yaliyotokea katika mkoa wa Mara na mengi ya mauaji hayo kutoripotiwa kabisa katika vyombovya habari pengine ni kutokana na waandishi wa habari kutoona umuhimu ama kutofuatiliamatukio hayo sambamba na viongozi kupuuza wakiwemo makamanda wa jeshilapolisi wa kanda maalum Tarime /Rorya na mkoa wa Mara.

Kabla ya kuwanyooshea vidole viongozi hao hebu kwanza nianze na sisi wenyewe kama waandishi wa habari ambaotumekuwa tukisikia matukio ya watu kuuawa na kutofuatilia huku tukifuatilia habari za vikao na mabaraza ya madiwani na kikutano ya wabunge kwa kuwatunajua kuna posho huko.


Hivi mtu kuuawa haijalishi kipato chake, mtanzania mwenye haki na thani ya kuishi kamabinabamu anauawa usitake kuandika habari hiyo na badala yake siku hiyo unaandika habari ya mbunge ama diwani katoa ahadi ya kukarabati barabara ama kachangia ujenzi wa sekondari, kweli hiyo ndiyo dhamani tuliyonayokatika kuielimisha, kuihabarisha Jamii ya watanzania kamawana habari?

Kwa upande wa viongozi watawala na makamanda na jeshila polisi, Kuna badhi ya matukio yakitokea hujitahidi kutoa taarifa kwa waandishi hata kwa kuwatafuta kwasimu, lakini baadhi ya matukio yakiwemo mauaji wa watu wenye kipato kidogo ambao bndio watanzania halisi na walio wengi wenye mchango mkubwa katika taifa lao, wanaoiweka serikali madarakani kuupuuzwa na kutotolewa taarifa endapo hakuna mwandishi naliyefuatilia amakuuliza juu ya mauaji hayo pengine kwakutopata dokezojuu ya tukiohilo.

Viongozi na waandishi wa Habari hatuwatendei haki watanzania walio wengi.