Wednesday, March 24, 2010

VIONGOZI WETU

Umefika wakti wa kuambiza ukweli kwani kila mtu katika nafasi yake anao uwezo wa kufanya kama siyo kuchangia katika jamii yake. kuna viongozi wanaodhani kuwa wanamuenzi Baba wa taifa Mwalimu julius K. Nyerere kwa kuwa katika chama au kubakia katika itikadi fulani, hii siyo kweli na ni wenda wazimu. Sina budi kuwaambia adhanie amesimama angalie asianguke.

Mwalimu alisema " heshima ya mtu haitokani na mali yake, cheo au elimu bali utu wake" pia wapo viongozi wanaodhani kuwa baba wa taifa ni mali yao japo ukiangalia mambo wanayoyafanya ni tofauti kabisa.

Tuesday, March 9, 2010

Kuhamisha Wafugaji Tarime Siyo Suluhisho- Uharifu

Kwa mara nyingine narudia kusema, hakuna njia moja katika kutatua matatizo, lakini nakubaliana na kauli ya kuwa kukimbia matatizo siyo njia ya kuepuka matatizo, haya ni maneno ya wahenga ambao walinena.

Kauli ya mkuu wa mkoa wa Mara kanari Enoce Mfuru ya kusema kuwa wafugaji walio katika wialya ya |Tarime wahamishwe kama njia ya kupunguza vitendo vza wizi wa mifugo na mauaji nasema kamwe siyo njia wala suluhisho la matatizo ya Tarime.

Tarime imekuwa katika hali ya machafuko kutokana na kilimo cha Bangi, Uhasama wa kugombania ardhi na mipanga ya asili iliyowekwa na mkoloni, kulipiza kisasi dhidi ya uhasama wa siku nyingi na wizi wa mifugo unaofanywa na baadhi ya wananchi wa wilaya hiyo.

Kilimo cha bangi kimechangia kwa kiwango kikubwa na kufanya wananchi wa wilaya ya Tarime wakiwemo vijana ambao kwa kiasi kikubwa wameathiriwa na uvutaji wa Bangi.

Kuwahamisha wananchi hao na kuwapeleka katika wilaya za Bunda, Musoma vijijini, na Serengeti haitawabadilisha tabia wala kuacha vitendo vya uharifu.

Kuhamisha wafugaji haina maana kuwa wafugaji ndiyo wezi bali serikali inapaswa kudhibiti wizi na vitendo vya uharifu na siyo kuhamisha wafugaji.

Kama wilaya ya Serengeti hali ya usalama na imewezekana kwa Tarime inashindikana VIPI???????.

Waziri mkuu aliyepita Edward Lowassa alikuwa na nia wa kweli katika kutatua matatizo ya Tarime kwa njia shirikishi ambapo wananchi walipewa fursa ya kutoa mchango wao juu ya kumaliza/ mgogoro huo hatua ambayo imetelekezwa na kutumia nguvu za dola kwa kuongoze maaskari ambao hawanakuleta mabadiliko yoyote.

LOWASSA KWA HILI UTAKUMBUKWA SANA NA WANATARIME.

Sunday, March 7, 2010

Mauaji Mara Serikali haijadhamilia kuyakomjesha.

Ni wahenga walisema ''usipoziba ufa utajenga ukuta, na udongo upasnde ugali maji, bila kusahau samaki mkuje angali mbichi.'' Metahli hizi zote zinamaana kubwa katika hali ya maisha ya wakazi wa mkoa wa Mara.

Kadharika wananuchumi wanasema hakuna njia sahihi ya kukuza au kuboresha uchumi isipokuwa njia yoyte ile itakayokuwa na mafanikia kwa wakati furani kutokana na hali halisi ya maisha na mweleke wa wakati huo.

Kumekuwa na mauaji ya mara kwa mara mkoani Mara huku serikali ikiwa imeweka askari polisi na kuunda kanda maalumu ya mkoa wa kipolisi Tarime / Rorya pasio mafanikio. Tena baada ya mkoa huo kuundwa matukio yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku.

Serikali inajua ukweli kuwa wananchi wa Tarime walisahaulika hadi kujiona kuwa hawapo Tanzania na kuanza kujifanya mabo wanavyotaka.

Pia kuweka askari bila kuangalia chanzo cha machafuko hayo siyo suluhisho wala ufumbuzi la tatizo hilo la wakazi wa Mara na mauaji yanaoendelea siku hadi siku.

Naamini serikali ikiwashirikisha wakaazi wa Mara kama walivyo wakweli na wawazi wenyewe watatoa ufumbuzi wa kukomesha hali hiyo tena bila gharama kubwa wala kuumiza wananchi kwa namna yoyote ile.

Serikali ikubali ushauri na itumie uongozi shirikishi, wananchi wahusike kutatua matatiyo yao wenyewe kama ilivyo adhina ya dhamira ya kuanzishwa kwa serikali za mitaa hapa nchini ya kurejesha madaraka mikononi mwa wananchi wenyewe. Sasa mbona mnayang'ang'ania hamtaki kuwaachia / kuwashirikisha wana - Mara katika kutafuta ufumbuyi.

Pia viongozi waongoze na wafuate mifano yab viongozi waliotangulia, Hapa siktasita Kumta Aliyekuwa waziri wa Mambo ya ndani ya nchi miaka ya 90 katika serikali ya awamu ya pili Augostino Ryatonga Mrema ambae aliweza kutuliza wilaya ya Serengeti Mkoani Mara ambayo ilikuwa tishio kubwa kwa usalama wa raia, mali zao na hata wageni tena ilikuwa hatari zaidi ya mara kumi ukilinganisha na Tarime inayohangaisha watu na kuharibu sifa ya Tanzania kwa kuhofia kuwa Mara ni hatari kiasi hicho. kwa wakati huo ambapo hadi sasa Serengeti ni swali.

Mrema bado yupo kwa nini asitumike.

MARA NI IMARA NA SIYO TISHIO.