Sunday, March 7, 2010

Mauaji Mara Serikali haijadhamilia kuyakomjesha.

Ni wahenga walisema ''usipoziba ufa utajenga ukuta, na udongo upasnde ugali maji, bila kusahau samaki mkuje angali mbichi.'' Metahli hizi zote zinamaana kubwa katika hali ya maisha ya wakazi wa mkoa wa Mara.

Kadharika wananuchumi wanasema hakuna njia sahihi ya kukuza au kuboresha uchumi isipokuwa njia yoyte ile itakayokuwa na mafanikia kwa wakati furani kutokana na hali halisi ya maisha na mweleke wa wakati huo.

Kumekuwa na mauaji ya mara kwa mara mkoani Mara huku serikali ikiwa imeweka askari polisi na kuunda kanda maalumu ya mkoa wa kipolisi Tarime / Rorya pasio mafanikio. Tena baada ya mkoa huo kuundwa matukio yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku.

Serikali inajua ukweli kuwa wananchi wa Tarime walisahaulika hadi kujiona kuwa hawapo Tanzania na kuanza kujifanya mabo wanavyotaka.

Pia kuweka askari bila kuangalia chanzo cha machafuko hayo siyo suluhisho wala ufumbuzi la tatizo hilo la wakazi wa Mara na mauaji yanaoendelea siku hadi siku.

Naamini serikali ikiwashirikisha wakaazi wa Mara kama walivyo wakweli na wawazi wenyewe watatoa ufumbuzi wa kukomesha hali hiyo tena bila gharama kubwa wala kuumiza wananchi kwa namna yoyote ile.

Serikali ikubali ushauri na itumie uongozi shirikishi, wananchi wahusike kutatua matatiyo yao wenyewe kama ilivyo adhina ya dhamira ya kuanzishwa kwa serikali za mitaa hapa nchini ya kurejesha madaraka mikononi mwa wananchi wenyewe. Sasa mbona mnayang'ang'ania hamtaki kuwaachia / kuwashirikisha wana - Mara katika kutafuta ufumbuyi.

Pia viongozi waongoze na wafuate mifano yab viongozi waliotangulia, Hapa siktasita Kumta Aliyekuwa waziri wa Mambo ya ndani ya nchi miaka ya 90 katika serikali ya awamu ya pili Augostino Ryatonga Mrema ambae aliweza kutuliza wilaya ya Serengeti Mkoani Mara ambayo ilikuwa tishio kubwa kwa usalama wa raia, mali zao na hata wageni tena ilikuwa hatari zaidi ya mara kumi ukilinganisha na Tarime inayohangaisha watu na kuharibu sifa ya Tanzania kwa kuhofia kuwa Mara ni hatari kiasi hicho. kwa wakati huo ambapo hadi sasa Serengeti ni swali.

Mrema bado yupo kwa nini asitumike.

MARA NI IMARA NA SIYO TISHIO.

No comments:

Post a Comment