Tuesday, March 9, 2010

Kuhamisha Wafugaji Tarime Siyo Suluhisho- Uharifu

Kwa mara nyingine narudia kusema, hakuna njia moja katika kutatua matatizo, lakini nakubaliana na kauli ya kuwa kukimbia matatizo siyo njia ya kuepuka matatizo, haya ni maneno ya wahenga ambao walinena.

Kauli ya mkuu wa mkoa wa Mara kanari Enoce Mfuru ya kusema kuwa wafugaji walio katika wialya ya |Tarime wahamishwe kama njia ya kupunguza vitendo vza wizi wa mifugo na mauaji nasema kamwe siyo njia wala suluhisho la matatizo ya Tarime.

Tarime imekuwa katika hali ya machafuko kutokana na kilimo cha Bangi, Uhasama wa kugombania ardhi na mipanga ya asili iliyowekwa na mkoloni, kulipiza kisasi dhidi ya uhasama wa siku nyingi na wizi wa mifugo unaofanywa na baadhi ya wananchi wa wilaya hiyo.

Kilimo cha bangi kimechangia kwa kiwango kikubwa na kufanya wananchi wa wilaya ya Tarime wakiwemo vijana ambao kwa kiasi kikubwa wameathiriwa na uvutaji wa Bangi.

Kuwahamisha wananchi hao na kuwapeleka katika wilaya za Bunda, Musoma vijijini, na Serengeti haitawabadilisha tabia wala kuacha vitendo vya uharifu.

Kuhamisha wafugaji haina maana kuwa wafugaji ndiyo wezi bali serikali inapaswa kudhibiti wizi na vitendo vya uharifu na siyo kuhamisha wafugaji.

Kama wilaya ya Serengeti hali ya usalama na imewezekana kwa Tarime inashindikana VIPI???????.

Waziri mkuu aliyepita Edward Lowassa alikuwa na nia wa kweli katika kutatua matatizo ya Tarime kwa njia shirikishi ambapo wananchi walipewa fursa ya kutoa mchango wao juu ya kumaliza/ mgogoro huo hatua ambayo imetelekezwa na kutumia nguvu za dola kwa kuongoze maaskari ambao hawanakuleta mabadiliko yoyote.

LOWASSA KWA HILI UTAKUMBUKWA SANA NA WANATARIME.

No comments:

Post a Comment