Wednesday, November 4, 2009

Waikizu ni wakulima/ wafugaji na wawindaji - Mara

jaji Warioba akitoa zawadi kwa niaba ya rais Benjamini William Mkapa - Nyamuswa.

Wanawito wasichana wa parokia ya Nyamuswa wakiserebuka katika kanisa wakati wa misa ya upandirisho wa Pius Msereti.

Wakristo wa parokia ya Nyamuswa Ikizu wakitoa zawadi ya ng'ombe kwa padre pius Msereti kama ishara ya kabila hilo ambalo ni wakulima, wafugaji na wawindaji mashuhuri hapa nchini.



Kabila la WAIKIZU wanaoishi mkoani Mara ni maarufu kwa kulima mzao la Mihogo kwa ajili ya chakula, na wafugaji wa mbuzi, kondoo na Ng'ombe kuhu kabila hilo likiwa maarufu kwa UWINDAJI wa wanyama pori.

Kabila hilo ambalo desturi zake ni za Kijamaa ni kabila maarufu mkoani Hapa ambalo hujulikana kwa kutokuwa na majivuno, bali watu wake hufanya kazi kwa ushirikiano hasa wakati wa msimu wa kilimo ambapo watu hulima mara nyingi kwa ushirikiano (LISAGA)kwa kabila hilo.

Pamoja na kuwa wawindaji, pia wamepata padre wa kwanza katika Parokia ya Ikizu - Nyamuswa (Padre Pius Msereti)

NI JUKUMU LA VIONGOZI WA DINI KUKEMEA UFISADI- ASKOFU

Askofu Michael musongazila (wa pili Kulia)na wa pili Kushoto ni Padre pius msereti mara baada ya Upadirisho- Nyamuswa Ikizu

Jaji Joseph Sinde Warioba akimpongeza Padre mpya Pius Msereti Mara baada ya kupadirishwa, Picha na Robinson Wangaso - Mara



Kanisa katoliki limesema ni jukumu la viongozi wa kanisa hilo kukemea vitendo viovu vinavyofanywa na baadhi ya viongozi hapa nchini ukiwemo ufisadi ili kuweza kuving'oa, kuvibomoa na kuviangamiza.

Kauli hiyo hiyo ilitolewa Julai 9 mwaka huu 2009 na askofu wa kanisa Katholiki jimbo la Musoma mhashamu Michael Msonganzila katika sherehe za upadirisho wa padre mpya Pius Msereti uliyofanyika katika parokia ya Nyamuswa - Ikizu wilayani bunda mkoani Mara.

Askofu Msonganzila alisema kanisa haliandai wagombea wa nafasi mbalimbali za siasa kama ilivyodaiwa na baadhi ya wanasiasa bali linaandaa waamini wake kushiriki katika uchaguzi ujao kwa umakini na kujiepusha na vitendo vya rushwa na kuchagua viongozi wasiyo faa.

"Ni wajibu wa viongozi wa kanisa Kung'oa, kubomoa na kuangamiza kwa kukemea maovu kwa neno la mungu na siyo kukaa kimya vikiwemo vitendo vya ufisadi" alisema Msonganzila.

Alisisitiza kuwa kamwe kanisa halitakaa kimya huku maovu yakiendelea katika jamii na wanachi wakiwa wanataabika kwani seriakli ya tanzania haina dini na wala serikali hiyo siyo ya dini yoyote.

Katika hatua nyingine alisema mapigano yanayoendelea katika wilaya ya Tarime na Rorya yanatokana na ugumu wa mioyo ya wanachi hao na viongozi wa dini inapaswa wayakemee pasipo kuogopa upande wowote ule.

Alisema ni hali ya kusikitisha kuona watu wanauwana bila hatia huku hali hiyom ikiendelea kufumbiwa macho.

Upadrisho huo wa padre Pius Msereti wa kwanza katika Parokia ya Nyamuswa na ni padre wa kwanza kutoka katika kabila la WAIKIZU na umehudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo mama Maria Nyerere, Waziri mkuu wa zamani Jaji Joseph Sinde Warioba ambae pia walitoa zawadi kwa niaba ya rais mstaafu wa awamu wa tatu Benjamin William Mkapa na viongozi mbalimbali waandamizi waserikali na vyama mbalimbali vya siasa.Kwa hili pia namshukru shakila omary kwa ushauri wake na mchango wa mawazo aliyotoa na Annastazia kutoka SAUT.



href="http://1.bp.blogspot.com/_-mB36LBfMg4/SvFQTyy6xxI/AAAAAAAAABU/EgcstdgzgO
/s1600-h/DSC01302.JPG">



,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,mwisho,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Waikizu wapata Padre wa Kwanza - Mara


Mama Maria Nyerere akipongeza padre pius Msereti mara baada ya kupokea daraja la upadre katika parokia ya Nyamuswa- Ikizu











Mapadre wa jimbo la Musoma wa kushoto (Mzungu) kutoka kwa pius Msereti ni paroko wa parokia ya kiabakari padre Voichek Adamu





Padre mpya Pius Msereti (kushoto) akisaini cheti cha upadrisho mbele ya Mwashamu askofu Michael(kulia) Msongazila wa jimbo Katholiki Musoma wa katikati Padre Chegere katibu wa askofu.



Tarehe 9 Julai ya mwaka 2009 ni siku muhimu na ya kumbukumbu muhimu kwa Kabila la waikizu kutokana na tukio la kihistoria ambayo haitabadilishwa na mtu yeyeote kutokana na umuhimun wake. Kwa mara ya kwanza siku hiyo kabila la Waikizu ambao wanaishi mkoani Mara, licha ya kuwa na viongozi mashuhuri wa kisiasa Nchini wasliowahi kushika nyadhifa mbalimbali akiwemo Waziri mkuu wa zamani na makamu wa kwanza wa rais wa Serikali ya awamu ya pili ambae pia aliwahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikli, Jaji Joseph Sinde Warioba, Waziri wa Kilimo chakula na Ushirika wa sasa Stephen Masatu Wasira, aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha wafanyakazi nchini marehemu Peter Nyamuhokya na viongozi wengineo, wamepata Padre Pius Msereti kwa mara ya kwanza.

Msereti anaonekana kuwa kiongozi wa kihistoria katika kabila hilo kutokana na Mambo ya imani kuwa na umuhimu wa pekee katika jamii ambapo sherehe ya upadirisho huo ilihudhuriwa na watu wenge huku rais mstaafu wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Benjamin willia Mkapa akiwakilishwa na Jaji warioba, Mama MAria Nyerere na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali za kitaifa wakishuhudia tukio hilo.