Wednesday, November 4, 2009

Waikizu ni wakulima/ wafugaji na wawindaji - Mara

jaji Warioba akitoa zawadi kwa niaba ya rais Benjamini William Mkapa - Nyamuswa.

Wanawito wasichana wa parokia ya Nyamuswa wakiserebuka katika kanisa wakati wa misa ya upandirisho wa Pius Msereti.

Wakristo wa parokia ya Nyamuswa Ikizu wakitoa zawadi ya ng'ombe kwa padre pius Msereti kama ishara ya kabila hilo ambalo ni wakulima, wafugaji na wawindaji mashuhuri hapa nchini.



Kabila la WAIKIZU wanaoishi mkoani Mara ni maarufu kwa kulima mzao la Mihogo kwa ajili ya chakula, na wafugaji wa mbuzi, kondoo na Ng'ombe kuhu kabila hilo likiwa maarufu kwa UWINDAJI wa wanyama pori.

Kabila hilo ambalo desturi zake ni za Kijamaa ni kabila maarufu mkoani Hapa ambalo hujulikana kwa kutokuwa na majivuno, bali watu wake hufanya kazi kwa ushirikiano hasa wakati wa msimu wa kilimo ambapo watu hulima mara nyingi kwa ushirikiano (LISAGA)kwa kabila hilo.

Pamoja na kuwa wawindaji, pia wamepata padre wa kwanza katika Parokia ya Ikizu - Nyamuswa (Padre Pius Msereti)

NI JUKUMU LA VIONGOZI WA DINI KUKEMEA UFISADI- ASKOFU

Askofu Michael musongazila (wa pili Kulia)na wa pili Kushoto ni Padre pius msereti mara baada ya Upadirisho- Nyamuswa Ikizu

Jaji Joseph Sinde Warioba akimpongeza Padre mpya Pius Msereti Mara baada ya kupadirishwa, Picha na Robinson Wangaso - Mara



Kanisa katoliki limesema ni jukumu la viongozi wa kanisa hilo kukemea vitendo viovu vinavyofanywa na baadhi ya viongozi hapa nchini ukiwemo ufisadi ili kuweza kuving'oa, kuvibomoa na kuviangamiza.

Kauli hiyo hiyo ilitolewa Julai 9 mwaka huu 2009 na askofu wa kanisa Katholiki jimbo la Musoma mhashamu Michael Msonganzila katika sherehe za upadirisho wa padre mpya Pius Msereti uliyofanyika katika parokia ya Nyamuswa - Ikizu wilayani bunda mkoani Mara.

Askofu Msonganzila alisema kanisa haliandai wagombea wa nafasi mbalimbali za siasa kama ilivyodaiwa na baadhi ya wanasiasa bali linaandaa waamini wake kushiriki katika uchaguzi ujao kwa umakini na kujiepusha na vitendo vya rushwa na kuchagua viongozi wasiyo faa.

"Ni wajibu wa viongozi wa kanisa Kung'oa, kubomoa na kuangamiza kwa kukemea maovu kwa neno la mungu na siyo kukaa kimya vikiwemo vitendo vya ufisadi" alisema Msonganzila.

Alisisitiza kuwa kamwe kanisa halitakaa kimya huku maovu yakiendelea katika jamii na wanachi wakiwa wanataabika kwani seriakli ya tanzania haina dini na wala serikali hiyo siyo ya dini yoyote.

Katika hatua nyingine alisema mapigano yanayoendelea katika wilaya ya Tarime na Rorya yanatokana na ugumu wa mioyo ya wanachi hao na viongozi wa dini inapaswa wayakemee pasipo kuogopa upande wowote ule.

Alisema ni hali ya kusikitisha kuona watu wanauwana bila hatia huku hali hiyom ikiendelea kufumbiwa macho.

Upadrisho huo wa padre Pius Msereti wa kwanza katika Parokia ya Nyamuswa na ni padre wa kwanza kutoka katika kabila la WAIKIZU na umehudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo mama Maria Nyerere, Waziri mkuu wa zamani Jaji Joseph Sinde Warioba ambae pia walitoa zawadi kwa niaba ya rais mstaafu wa awamu wa tatu Benjamin William Mkapa na viongozi mbalimbali waandamizi waserikali na vyama mbalimbali vya siasa.Kwa hili pia namshukru shakila omary kwa ushauri wake na mchango wa mawazo aliyotoa na Annastazia kutoka SAUT.



href="http://1.bp.blogspot.com/_-mB36LBfMg4/SvFQTyy6xxI/AAAAAAAAABU/EgcstdgzgO
/s1600-h/DSC01302.JPG">



,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,mwisho,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Waikizu wapata Padre wa Kwanza - Mara


Mama Maria Nyerere akipongeza padre pius Msereti mara baada ya kupokea daraja la upadre katika parokia ya Nyamuswa- Ikizu











Mapadre wa jimbo la Musoma wa kushoto (Mzungu) kutoka kwa pius Msereti ni paroko wa parokia ya kiabakari padre Voichek Adamu





Padre mpya Pius Msereti (kushoto) akisaini cheti cha upadrisho mbele ya Mwashamu askofu Michael(kulia) Msongazila wa jimbo Katholiki Musoma wa katikati Padre Chegere katibu wa askofu.



Tarehe 9 Julai ya mwaka 2009 ni siku muhimu na ya kumbukumbu muhimu kwa Kabila la waikizu kutokana na tukio la kihistoria ambayo haitabadilishwa na mtu yeyeote kutokana na umuhimun wake. Kwa mara ya kwanza siku hiyo kabila la Waikizu ambao wanaishi mkoani Mara, licha ya kuwa na viongozi mashuhuri wa kisiasa Nchini wasliowahi kushika nyadhifa mbalimbali akiwemo Waziri mkuu wa zamani na makamu wa kwanza wa rais wa Serikali ya awamu ya pili ambae pia aliwahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikli, Jaji Joseph Sinde Warioba, Waziri wa Kilimo chakula na Ushirika wa sasa Stephen Masatu Wasira, aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha wafanyakazi nchini marehemu Peter Nyamuhokya na viongozi wengineo, wamepata Padre Pius Msereti kwa mara ya kwanza.

Msereti anaonekana kuwa kiongozi wa kihistoria katika kabila hilo kutokana na Mambo ya imani kuwa na umuhimu wa pekee katika jamii ambapo sherehe ya upadirisho huo ilihudhuriwa na watu wenge huku rais mstaafu wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Benjamin willia Mkapa akiwakilishwa na Jaji warioba, Mama MAria Nyerere na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali za kitaifa wakishuhudia tukio hilo.

Friday, October 30, 2009

Picha - Mafunzo ya Internet Mwanza kwa waandishi

Mauaji ya Albino yanatokana na Asili.

Robinson Wangaso akiwa katika mafunzo ya internet

Pamoja na kupewa umuhimu na msukumo wa kisiasa mkubwa katika kushughulikiwa suala la mauaji ya Malbino nchini, mauaji hayo ni vigumu kukomeshwa kwa njia zinazotumika sasa kutokana na msingi kuwa yanatokana na jadi/asili ya watanzania na imani yao juu ya jamii hiyo.

Mauaji hayo ambayo yamekuwa yakiripotiwa kwa kiasi kikubwa katika kanda ya Ziwa mikoa ya Shinyanga, Mara, Kagera na Mwanza hususani wilaya za Geita, Magu, Misungwi, Sengerema na Kwimba.

Mikoa na wilaya hizo ambazo mauaji yamekithiri wengi wa wakazi wake wanakabiliwa na tatizo la ukosefu wa elimu ambalo limesababisha wao kujihusisha na vitendo vya kishirikina, ambapo wamekuwa wakienda kwa waganga wa jadi na kupigiwa ramli chonganishi.

Vitendo vya mauaji ya albino pia vimechangiwa na baadhi ya watu wanaojihusisha na shughuli za uvuvi na uchimbaji wa madini, ambapo wamekuwa wakiamini kuwa mvuvi akiingia na kiungo kimojawapo cha albino mfano nywele, damu, mfupa na ngozi kwenye mtumbwi wake hupata samaki wengi, hali kadhalika kwa mchimba madini.

Kufuatia imani hizo watu hao kwa asilimia ndio wanaochangia mauaji hayo kutokana na kutafuta vioungo hivyo kwa ajili ya shughuli zao hizo.

Lakini pia ongezeko la waganga wa jadi kwa asilimia kubwa nalo limechangia mauji ya albino, kutokana na kuwaagiza wafanyabiashara, wachimba madini na hata wavuvi baadhi ya viungo vya aklbino ili waweze kufanikiwa katika shughuli zao na hatimaye kuwa matajiri.

Mwenyekiti wa chama cha albino Mkoa wa Mwanza Bw. Alfed Kapole amesema kufuatia kuibuka kwa wimbi la mauiji yanayowalenga, hivi sasa wamekuwa wakiishi maisha magumu ya kujificha na hivyo kushindwa kufanya kazi za kujipatia kipato, sanjari na watoto kushindwa kwenda shule kwa kuhofia kuuawa.

“ Hata tunapokwenda hosptali au kwenye vituo vya afya baadhi ya wauguzi wamekuwa wakitunyanyapaa, yaani hawataki kabisa kugusana na sisi hivyo kushindwa kutoa tiba sahihi kwa mgonjwa, kwa ujumla hatuna sehemu ambayo tunaweza kupata msaada, kwani hata kwenye jamii inayotuzunguka kila wanapomwona albino wamekuwa wakishangilia kwa kumwita “DILI” sijui tukaishi wapi maana tumekuwa kama wakimbizi ndani ya nchi yetu” alisema Kapole.

Kutokana na mauji hayo hadi sasa takribani zaidi ya albino 44 wameuwa, ambapo ni kesi moja tu ndiyo imetolewa hukumu na watu watatu kuhumiwa kunyongwa hadi kufa mkoa Shinyanga.

kutokana na serikali kuona umuhimu wa kushughulikia tatizo hilo, waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda alitoam uamuzi wa kufuta vibali vya waganga wote wa Tiba za jadi nchini ikiwa kama mkakati mojawapo wa kupambana na mauaji hayo.

Licha ya kufutwa kwa Leseni hizo, imani kuwa viuongo vya Albino vinaleta utajili itakuwa imefutwa katika akili za jamii hiyo na na itasaidia kuleta uelewa miongoni mwa wachimbaji madini, wavuvi na wafanyabiashara kuwa albino ni ulemavu kama ulivyo ulemavu mwingine?.Mfano wa Jamii kwanza na maggid Mjigwa ni mfano mzuri wa uwazi na uwajibikaji

watanzania tumekuwa wepesi kukimbilia kuiga mambo ya kigeni na kuacha mila zetu, kwa kufuata hata mambomyasiyofa, hili la mauaji kwa nini tusielewe kuwa Imani hizo zimepitwa na wakati na tumebaki kulingángánia.

Nimeweza kuongea na wazee wengi kutoka kanda ya ziwa ambao wanasema zamani Albino alionekana kama mkosi katika jamii na mazishi yake yalifanyika kwa siri pasipo watu kujua amabop siyo ndugu ama marafiki wa karibu, na baadhi yao walithubutu hata kuwanyoga watoto wadogo wakati walipozaliwa na endapo mkunga alibaini kuwa mtoto huyo alikuwa na ulemavu wa aina hiyo. Wizara ya afya tanzania

Thursday, October 29, 2009

Lake zone Journalist Internet training Bomba – Day 4.

As I’m going ahead with the Internet training, I discover that, as a journalist there is a lot to do by the Internet.

About blogger linking you can have much information from your fellow friends. Blogger is another way of gating news/ information which is very necessary like Wangari Maathai a Kenyan journalist.Also i like the way we work as team work other participant eg Jane Kajoki

Wednesday, October 28, 2009

Internet Muhimu

The way we proceed with the Internet Training, things going smooth compare when we started on monday 26TH October, 2009.

Almost now we can use the internet for searching news / information as the source due to the Internet Lake Journalist Training which takes place at BoT Insitutite in Mwanza City.

Through my exprience, journalists should learn much about how to use the Internet for the purpose of their duties.

Robinson Wangaso
Rhobinson_wangaso@yahoo.co.uk
+255784301526/+255765632944

Tuesday, October 27, 2009

Nice training

Habari Wazee

Today was a good second day for training, but my effort went down after loosing all data about blogger. Obviously the training went well especially the website we visited and searching information was very interested for me and I hope so for other participants.

The challenges are much practices about what we learn for our own daily duties in the field / office as journalists in-order to be aware about the Technology changes/ internet uses.

Thanks Mr. Peik Johansson for a nice lecture.

Robinson Wangaso
From Mara Region
Rhobinson_wangaso@yahoo.co.uk,
Mobil; +255784301526/+2557656344.

Mara Journalist going online

My name is Robinson Wangaso, Journalist from Mara Regional Press Club. . I am working with Victoria Fm radio and Business Times LTD as reporter in Mara (Times FM radio and Majira news paper).

I am attending the internet training for Lake zone Journalist held at Bank of Tanzania Training Institute (BoT) in Mwanza about how internet has changed society, different ways of using internet; for example, as a global library, global news room, phone directory, encyclopedia and also as a chat room, discussion groups or for TV, Radio, music and all kinds of games and gambling.

For one week, the training on internet will enlarge my awareness on the internet uses much than communicating and sending news stories as previously.

I am advising all journalist in Tanzania to Learn much about Internet and other professionalism studies.
Robnson Wangaso
Cell: +255 784 301526 and +255 765632944,
Email: Rhobinson_wangaso@yahoo.co.uk