Sunday, September 19, 2010

SIKU TISINI ZA MASOMONI SWEDEN.

Na Robinson Wangaso - Sweden





Hakika kutembea ni kujifunza, pampja na kuwa nilikuwa nchi Swedeni kwa ajili ya masomo lakini kuna elimu kubwa niliyoipata nje ya darasani kwa kujifunza mambo mengi yakiwemo utunzaji wa mazingira, jinsi watu wanavyojichukulia au kujiheshimu na kutojiheshimu kwa nkuwa wapo ulaya.

Kwangu kwenda ulaya siyo jambo muhimu, muhimu ni matokeo baada ya kutoka Ulaya nini nitajifunza na ni namna gani nitaweza kubadilisha hali fulani katika maisha na namna ya kusaidia jamii ya Watanzania.

Wapo walioenda mbali zaidi na hata kutaka kukana desturi zao wakidhani ulaya ndiyo mambo yote, lakini nilichokibaini ni kuwa WAZUNGU wanayo hamu kubwa ya kujifunza kutoka kila kona hata kwa WAAFRIKA ambao tumekuwa kujijidharau kila siku.

Haba baadhi ya Watanzania wakiwa nchini Sweden

No comments:

Post a Comment