Thursday, January 21, 2010

USHIRIKINA KAZINI / MAOFISINI JAMANI

Ni kweli kwa siku za hivi karibuni, kumekuwepo na malalamiko mengi dhidhi ya vitendo vya kikatili na kinyama dhidi ya mauaji ya walemavu wa ngozi (Albino)kutokana na vifO vyenye simanzi na masikitiko makubwa DHIDI YA BUNADAMU WENZETU.

Hali hii inatokana na wasomi tulionao kuwa na imani potofu juu ya ushirikina. Kama Mtu aliyesoma na kufuzu shahada/ stashahada, bado anaamini juu ya ushirikina. Mtu kama huyo kabla ya kuanza kazi anaanzia kwa mganga wa JADI ndipo aanze kazi. Wengine huenda mbali zaidi na hata kudriki kupeleka katika ofisui wanazofanyia kazi waganga ili wazindiki ofisi hizo wakidhani pasipo kufanya hivyo hawatakuwa salama. Je, hivi tunao wasomi au ni vyema turudi kwa Mababi na Mabibi zetu tuwaachie ofisi waziendeshe? kwani pamoja na kusomabado tunaamini bila ushirikina mambohayaendi.

Kama msomi anaamini ushirikina, anaenda kwa mganga kabla ya kuanza kazi au akazindike ofisi, Unadhani kati ya mganga na Mtu huyo anaejiita Msomi nani aachiwe ofisi. Nasisitiza hili kwa sababu huwezi kujua kesho mganga atamshauri nini huyo mwajiriwa mwenye kutegemea mganga na pasipo Ushirikina hajiiaminin kuwa yupo kazini.

Naombeni ushauri na mawazo yenu juu ya suala hili. Hawa wasomi Tegemezi, hawatufai kamwe kuendelea kuwa nao katika ofisi yoyote ile ni kuwa na mtu hatari kwa maendeleo ya taifa. Ni msimamo na Mtazamo wangu tu, Nawe toa wako.

Robinson Wangaso

No comments:

Post a Comment